JENGO LA 3 LA ABIRIA JNIA KUONGEZA CHACHU YA UCHUMI
JENGO la tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TBIII) litaongeza chachu ya kukua kwa uchumi wa nchi, imeelezwa.
Hayo yamesemwa leo na Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipozindua jengo hilo ambalo sasa limeanza kutumika kwa safari za nje ya nchi baada ya kukamilika kwake.